ASKOFU Severine Niwe-Mugizi wa Jimbo Katoliki Rulenge-Ngara,
amekemea tabia iliyoanza kujitokeza katika siku za hivi karibuni ya
baadhi ya watu hususani vijana, kuabudu mashetani kupitia Imani ya
Freemason.
Ametoa kauli hiyo katika Ibada ya Misa Takatifu kwenye Dominika ya
sita ya Pasaka ambapo vijana 250 wamepata Sakramenti ya Kipaimara. Ibada
hiyo imefanyika katika Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu-
Buseresere Askofu Niwe-Mugizi amebainisha kuwa ni aibu jamii ya sasa,
hususani vijana kuamua kuishi kadiri watakavyo, wakidhan kuwa hakuna
taratibu na miongozo ya Kanisa. “Wapo watu ambao wanapata mali kwa njia
za kishirikina na hatimaye wanashangiliwa na jamii kwa ushindi
walioupata,” amesema. Akizungumza kwa msisitizo, amesema jamii ya sasa
imehalalisha maovu na wale wanaoyatenda wanashangiliwa. “Inashangaza
kuona watu wanashangiliwa kwa maovu badala ya kushangiliwa kwa mema, hii
siyo sahihi,” amesema. Imani ya kishetani Askofu Niwe-Mugizi ameendelea
kueleza kuwa kadiri siku zinavyosonga, ndivyo vijana wanavyoendelea
kuharibika. “Jamii ya sasa hushawishika kirahisi na kujiingiza katika
tabia chafu na mbaya zaidi madawa ya kulevya na hatima wanajikuta
wanatumbukia katika dimbwi la kuabudi mashetani (Freemason) ili
wajipatie mali za haraka bila kutafakari madhara yake,” anasema Amewaasa
vijana hao waliopata Sakramenti ya Kipaimara kuwa makini na mambo ya
ulimwengu na kuepuka kudanganyika, kushawishika hasa kupenda mali zisizo
za halali. Kuhusu siasa Katika hatua nyingine Askofu Niwe-Mugizi
amegusia suala zima la Wakristo Wakatoliki kudharau masuala ya siasa na
kufikiri kuwa wao siyo sehemu ya maisha hayo. “Mwaka huu Mchakato wa
Mabadiliko ya Katiba, baada ya chaguzi za Serikali za Mitaa na uchaguzi
mkuu mwakani. Kuna tatizo la baadhi ya waamini kutoshiriki,” akasema
Amekemea tabia ya baadhi ya waamini kubweteka na kutotimiza wajibu wao
kihalali wa kwenda kupiga kura kuwachagua viongozi wanaofaa bila kujali
itikadi ya vyama vyao. “Tendo hili la mtu kutoenda kupiga kura ni dhambi
ya kutotimiza wajibu,” amesema.
Friday, June 6, 2014
imani za Freemason
By Unknown at 12:38 AM
No comments
Related Posts:
download wimbo Bwana ni ngome yangu MT Theresia Arusha … Read More
dowload wimbo Mt Theresia Arusha - Nimeonja pendo lako hapa … Read More
Pope prays at Israel's West Bank separation barrier The Pope rested his head against Israel's separation barrier as he prayed Pope Francis has prayed at the concrete barrier Israel is building in and around the West Bank during his three-day tour of the Middle East. Th… Read More
DID YOU KNOW? You can use steel wool to: Fill a screw hole that has become too big for the screw. Stuff the hole with steel wool and re-insert the screw. Make an instant pincushion. Stuff an old sock wit… Read More
lets pray May your Spirit, O Lord, we pray, imbue us powerfully with spiritual gifts, that he may give us a mind pleasing to you and graciously conform us to your will. Through our Lord Jesus Christ, your Son, who lives and reigns with… Read More
0 comments:
Post a Comment