ASKOFU Severine Niwe-Mugizi wa Jimbo Katoliki Rulenge-Ngara,
amekemea tabia iliyoanza kujitokeza katika siku za hivi karibuni ya
baadhi ya watu hususani vijana, kuabudu mashetani kupitia Imani ya
Freemason.
Ametoa kauli hiyo katika Ibada ya Misa Takatifu kwenye Dominika ya
sita ya Pasaka ambapo vijana 250 wamepata Sakramenti ya Kipaimara. Ibada
hiyo imefanyika katika Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu-
Buseresere Askofu Niwe-Mugizi amebainisha kuwa ni aibu jamii ya sasa,
hususani vijana kuamua kuishi kadiri watakavyo, wakidhan kuwa hakuna
taratibu na miongozo ya Kanisa. “Wapo watu ambao wanapata mali kwa njia
za kishirikina na hatimaye wanashangiliwa na jamii kwa ushindi
walioupata,” amesema. Akizungumza kwa msisitizo, amesema jamii ya sasa
imehalalisha maovu na wale wanaoyatenda wanashangiliwa. “Inashangaza
kuona watu wanashangiliwa kwa maovu badala ya kushangiliwa kwa mema, hii
siyo sahihi,” amesema. Imani ya kishetani Askofu Niwe-Mugizi ameendelea
kueleza kuwa kadiri siku zinavyosonga, ndivyo vijana wanavyoendelea
kuharibika. “Jamii ya sasa hushawishika kirahisi na kujiingiza katika
tabia chafu na mbaya zaidi madawa ya kulevya na hatima wanajikuta
wanatumbukia katika dimbwi la kuabudi mashetani (Freemason) ili
wajipatie mali za haraka bila kutafakari madhara yake,” anasema Amewaasa
vijana hao waliopata Sakramenti ya Kipaimara kuwa makini na mambo ya
ulimwengu na kuepuka kudanganyika, kushawishika hasa kupenda mali zisizo
za halali. Kuhusu siasa Katika hatua nyingine Askofu Niwe-Mugizi
amegusia suala zima la Wakristo Wakatoliki kudharau masuala ya siasa na
kufikiri kuwa wao siyo sehemu ya maisha hayo. “Mwaka huu Mchakato wa
Mabadiliko ya Katiba, baada ya chaguzi za Serikali za Mitaa na uchaguzi
mkuu mwakani. Kuna tatizo la baadhi ya waamini kutoshiriki,” akasema
Amekemea tabia ya baadhi ya waamini kubweteka na kutotimiza wajibu wao
kihalali wa kwenda kupiga kura kuwachagua viongozi wanaofaa bila kujali
itikadi ya vyama vyao. “Tendo hili la mtu kutoenda kupiga kura ni dhambi
ya kutotimiza wajibu,” amesema.
Friday, June 6, 2014
imani za Freemason
By Unknown at 12:38 AM
No comments
Related Posts:
NIGHT PRAYER In the name of the Father + and of the Son, and of the Holy Spirit. Amen. Lord Jesus Christ, my God, I adore You and thank You for all the graces You have given me today. I offer You my sleep and all the moments of this ni… Read More
Mary has the authority over the angels"Mary has the authority over the angels and the blessed in heaven. As a reward for her great humility, God gave her the power and mission of assigning to saints the thrones made vacant by the apostate angels who fell away … Read More
Holy MaryHoly Mary, help those in need, give strength to the weak, comfort the sorrowful, pray for God's people, assist the clergy, intercede for religious. Mary all who seek your help experience your unfailing protection. Amen. … Read More
PRAYER FOR RELIEVING STRESS AND ANXIETY Lord, there has been too much change in my life recently, and I feel overwhelmed. Because I try to be a responsible person, I sometimes forget that it is unwise for me to allow my sense of duty to override my common sens… Read More
SAY THIS PRAYER BEFORE YOU LEAVE HOME TODAY Lord I need you; To guide me from all dangers from sudden deaths and accidents from all storms and lightening but mostly to guide me away from sin this day. Grant me your love and Joy May I remain faithful to you till the… Read More
0 comments:
Post a Comment